mambo

mambo

WEKA

WEKA

SULUM

SULUM

Pages

Saturday, December 14, 2013

JE, HAPA NI NANI ALIKUWA NA DHAMBI?


MCHUNGAJI alitangaza siku ya kuchangia pesa ya ujenzi wa kanisa. Waumini walijitokeza kwa wingi na kufanya changizo na kupatikana shilingi laki moja, na hapo MC aliwakamua kwelikweli.

Mchungaji alishukuru kwa kupata kiasi hicho cha pesa kwa ajili ya ujenzi. Ghafla waliingia majambazi sita na kuliteka kanisa. Hakuna aliyetoka na kuwataka kila mmoja kutoa pesa aliyonayo.

Majambazi yalikusanya huku wakawatisha kwa mapanga.

Waumini walitoa pesa zote ambapo zilipatikana shilingi milioni moja cash! 
Pesa hiyo wakamkabidhi mchungaji na kumwambia achanganye na zilizochangwa kwa hiari.


Jumla ikawa milioni moja na laki moja na kumwambia zote zikatumike kwenye ujenzi na baada ya zoezi hilo majambazi yalitoka huku yakiwataka waumini kuendelea na ibada.

Je, hapa ni nani alikuwa na dhambi? Kati ya waumini waliochangia laki moja kwa ajili ya ujenzi na kusema hawana pesa au majambazi waliochangisha mchango na kupata shilingi milioni moja?

No comments:

Post a Comment