Mama mkwe kamkuta jamaa sebuleni kapandisha hasira anadai ataua mtu.
MAMA KWE: Mwanangu kwani kuna nini jamani?
JAMAA: Leo namuua mwanao, mshenzi sana.
MAMA MKWE: Tulia jamani, kimetokea nini?
JAMAA: Mwanao mshenzi sana, nilikuwa nimesafiri, nikamtumia meseji kuwa
nakuja, eti bado leo nimefika nimemkuta na mwanaume kwenye kitanda
chetu, dharau gani hii, sikubali leo tunagawana majengo ya serikali,
yeye anaenda kulala Muhimbili mi naenda kulala Segerea
MAMA MKWE:
Subiri kwanza, mwanangu hayuko hivyo lazima kuna maelezo fulani kuhusu
hili ngoja nimuulize...mama mkwe akamfwata mwanawe na baada ya muda
akarudi sebuleni.
MAMA MKWE: Unaona, nilijua mimi lazima kuna sababu. Kumbe mwenzio hakupata ile meseji uliyomtumia.
JAMAA: ""enheeeeee...!
No comments:
Post a Comment