mambo

mambo

WEKA

WEKA

SULUM

SULUM

Pages

Sunday, October 12, 2014

MZEE NIMESHINDWA MIMI.



Mdada alienda kwa mtaalamu amuangalie mambo yake maana aliona mumewe ameanza kupunguza mapenzi. Baada ya kujieleza, mganga akatoa Laptop yake akaunganisha intanet kisha akaanza kugugo. Baada ya dakika kadhaa akiwa anaongea mwenyewe na kuonekana akiperuzi fesibuku na twira akainua kichwa;
MTAALAM: dada, tatizo lako nimeliona linahitaji fedha kiasi cha laki na nusu.
MDADA: He jamani hela yote hiyo ya nini?
MTAALAM: Mama mambo yamebadilika sana, siku hizi ili kuwasiliana na mizimu lazima uwe na intanet sasa  mimi hapa nimeweka WIFI na ni gharama maana ili ku'skype na mizimu inaweza ikanichukua hata wiki kumpata muhusika. Sasa hapo hiyo hela mama ni ya kulipia internet tu ili kupata maelezo ya matibabu yako
MDADA: Mzee nimeshindwa mimi.

No comments:

Post a Comment