mambo

mambo

WEKA

WEKA

SULUM

SULUM

Pages

Thursday, November 06, 2014

WOTE MNAJUA NILIFUNGWA MIAKA NANE

JAMAA  alifungwa miaka nane, alipofunguliwa akarudi kijijini kwao baada ya siku mbili akamwomba mwenyekiti wa kijiji aitishe mkutano maana alikuwa na neno la kusema. Watu wakahudhuria jamaa akakaribishwa kuongea. Akachukua sime lake lililokuwa limenolewa vizuri, akasimama na kuanza kutoa hotuba
MFUNGWA:  Wote mnajua nilifungwa miaka nanesasa nimerudi. Jambo la kusikitisha ni kuwa wakati niko jela kuna mtu akamchukua mke wangu na kumfanya wake. Sasa kwa vile yuko hapa mi naua halafu narudi jela. Baada ya kusema vile akanyanyua sime na kuanza kukaribia waliokuwa wakimsikiliza, wanaume saba wakatimka mbio ghafla. Jamaa akabaki kaduwaaa, kucheki, kaka zake wawili, mjomba wake, baba ake mdogo, na rafiki zake watatu.
 

No comments:

Post a Comment