mambo

mambo

WEKA

WEKA

SULUM

SULUM

Pages

Wednesday, December 24, 2014

KWELI YULE MJINGA



JOHN: Mke wangu ananidharau sana
NGONGO: Kivipi?
JOHN: Anasema eti hakuna mtu mjinga kama mimi duniani
NGONGO: Huyo mama hajaona wajinga nini? Ona, ngoja nimuite yule dereva wa kibajaji ndio ujue duniani kuna wajinga. ngongo akamuita yule dereva wa kibajaji
NGONGO: Aise hebu chukua hizi shilingi elfu mbili, nenda pale kwangu kaangalie kama nipo
KIBAJAJ: Ndio mzee.. Dereva akaondoka huyooo
NGONGO: Unaona John sasa ndio ujue kuna watu wajinga bwana
JOHN: Kweli yule mjinga, ningekuwa mimi ningechukua hela halafu ningekupigia simu nikuulize kama upo

No comments:

Post a Comment